Serikali inafanya juhudi kujaribu kuokoa familia ya watu wanne ambao wametekwa nyara nchini Ethiopia. Wafugaji wa mifugo kutoka Ethiopia wanataka mifugo wao walioibwa na wavamizi kutoka Turkana kurejesha mifugo hao kabla ya kuachiliwa kwa mateka hao. Mkuu wa wilaya ya Kibish Erick Wanayonyi anasema kwamba mazungumo yanaendelea kati ya serikali husika ili wanne hao waachiliwe huru.